
"Kiukweli kuzuiliwa kwa movie yangu kumeniletea matatizo sana, mipango yangu mingi imefeli na nimepata hasara zaidi ya shilingi mil.15 ambazo nilizitumia katika kufanya matangazo, na kufanya uzinduzi mikoani."
Akiizungumzia Bodi ya filamu Tino alisema-"Bodi ya filamu iache ukiritimba, kwasababu kila ninapofuatlia hawanipi majibu ya kueleweka, kila siku wananiambia nisubiri, wananiangusha sana coz kila muda unavyozidi kwenda ndivyo hasara juu yangu zinapoongezeka.
Ninachowaomba waniambie kipi kisichofaa katika filamu yangu nikiondoe ili niweze kuingiza sokoni."
Blog hii ilipojaribu kuwasiliana na katibu mkuu wa Bodi ya filamu Bi.Joyce Fisso kupitia simu ya kiganjani hakuweza kupatikana.
No comments:
Post a Comment